Matokeo ya Mitihani
Haraka · Sahihi · Rahisi

Wanafunzi, wazazi na walimu — angalia matokeo ya mtihani wako moja kwa moja. Mikoa yote Tanzania.

6,726+ Shule
11 Mikoa
Live Matokeo ya sasa

TAARIFA KUHUSU MATOKEO YA MOCK KIDATO CHA NNE (TASIDO)


Tunapenda kuwataarifu wadau wote wa elimu kuwa zoezi la uingizaji wa alama za Mtihani wa Mock Kidato cha Nne kwa mikoa ya Tabora, Singida, Iringa na Dodoma limekamilika kwa mafanikio.


Kwa sasa, hatua inayoendelea ni uchakataji na uhakiki wa matokeo hayo ili kuhakikisha yanakuwa sahihi na yenye ubora unaotakiwa kabla ya kutangazwa rasmi.


Matokeo rasmi yatatangazwa mara tu yatakapopata idhini kutoka kwa Idara za Elimu za mikoa husika. Matokeo hayo yataonesha namba za watahiniwa pekee bila majina yao, hivyo yatapatikana kwa uwazi kwa wadau wote bila kuhitaji neno siri (password).


Tahadhari: Tunawaomba wadau wote kuendelea kuwa na subira na kupuuza taarifa zozote zisizo rasmi kuhusu matokeo hayo mpaka yatakapotangazwa rasmi.

Ahsanteni kwa ushirikiano.


Imetolewa na FamNET.



Chagua Mkoa Wako
Mikoa 11 Tanzania Bara
💡 Jinsi ya kutafuta matokeo yako Bonyeza mkoa wako → chagua mtihani → chagua wilaya → tafuta shule yako. Matokeo yanaonekana bure, bila kusajili.