Wanafunzi, wazazi na walimu — angalia matokeo ya mtihani wako moja kwa moja. Mikoa yote Tanzania.
Tunapenda kuwataarifu wadau wote wa elimu kuwa zoezi la uingizaji wa alama za Mtihani wa Mock Kidato cha Nne kwa mikoa ya Tabora, Singida, Iringa na Dodoma limekamilika kwa mafanikio.
Kwa sasa, hatua inayoendelea ni uchakataji na uhakiki wa matokeo hayo ili kuhakikisha yanakuwa sahihi na yenye ubora unaotakiwa kabla ya kutangazwa rasmi.
Matokeo rasmi yatatangazwa mara tu yatakapopata idhini kutoka kwa Idara za Elimu za mikoa husika. Matokeo hayo yataonesha namba za watahiniwa pekee bila majina yao, hivyo yatapatikana kwa uwazi kwa wadau wote bila kuhitaji neno siri (password).
Ahsanteni kwa ushirikiano.
Imetolewa na FamNET.